- Nyumbani
- Huduma
- Taarifa
- Kuhusu
Huduma
Habari kuhusu kuishi Kenya
Habari kuhusu huduma za mitaani
Habari kuhusu pahali na jinsi ya kupata hati kama kibali cha kazi, leseni ya udereva
Usaidizi wa kufanya upya hati
Mkalimani atakwenda na wewe kukusaidia kupata huduma ya umma
Mahitaji ya Ustahiki
Huduma zote zilizoorodheshwa hutolewa bure
Huduma hutolewa kwa wakimbizi, wanaotafuta hifadhi na walionyanyaswa kijinsia (SGBV). Mikutano hupangwa wakati wa masaa ya kazi na siku za kazi, Jumatatu hadi Ijumaa, Saa 2 asubuhi hadi Saa 11 jioni - Kesi za dharura ambazo hutokea nje ya masaa rasmi ya ofisi huzingatiwa.
Upatikanaji wa Huduma
Huduma hupatikana pia kwa kupiga simu kwa nambari 0703848641. Simu zinaweza kupigwa baada ya masaa ya kazi, kwa kesi za dharura.
Kwa sababu ya ugonjwa wa COVID 19, huduma za kisheria na za ushauri hufanywa kwa mikutano iliyopangwa kwa kupiga simu kwa nambari iliyotolewa. Huduma zinapatikana bila rufaa.
Tafsiri ya lugha za Oromo, Somali, Sudan Kusini, Kiingereza, na Kiswahili hupatikana kila wakati katika ofisi zetu.
Huduma zinapatikana katika lugha zifuatazo kwa tafsiri ya simu - Kioromo, Somali, Sudan Kusini, Kiingereza na lugha za Kiswahili.
Watafsiri wa kike wanapatikana
Kiingilio cha pahali hapa kina njia panda
Pahala hapa pana wafanyikazi wa kike
Huduma zinapatikana Jumatatu hadi Ijumaa: Saa 2 asubuhi – Saa 11 jioni.
Ofisi zinafungwa siku za sikukuu za umma
Simu zinaweza kupigwa nje ya masaa ya kazi, kwa kesi za dharura.
Kwa sababu ya ugonjwa wa COVID 19, huduma za kisheria na za ushauri hufanywa kwa mikutano iliyopangwa kwa kupiga simu kwa nambari za RCK.
Utaratibu wa kutoa maoni na muda wa kujibu
Simu, barua pepe, ana kwa ana.
Haraka iwezekanavyo